Monday, June 14, 2010

KUKUMBUSHANA HUKU HADI HILI??

Kama tatizo litakuwa langu, basi kwa moyo mweupe kabisa naomba nisaidiwe kueleweshwa, lakini kiukweli kuna baadhi ya maadhimisho tunayoyasherekea binafsi sioni mantiki yake kabisa, kwasababu baada ya kuadhimisha, haturudi kuyashughulikia, au kama tunarudi kuyashughulikia si katika kiwango chenye tija.

Ndio maana najiuliza kuna maana gani sasa ya kusherekea na kukumbushana, kama si ufujaji tu wa pesa za wananchi na wahisani katika kufanya sherehe hizo, jambo ambalo kama pesa hizo zingetumika katika kushughulikia matatizo hayo yanayoendana na siku hiyo tunayoisherekea, inawezekana kabisa zikawa zimeleta mabadiliko makubwa katika kukomesha matatizo hayo.

Kwa mfano; siku si nyingi zilizopita tuliadhimisha siku ya malaria duniani, ambapo serikali, taasisi na asasi zingine zisizo za kiserikali walifanya maadhimisho mbalimbali katika mikoa mbalimbali nchini.

Labda kwa mfano tu nizungumzie taasisi moja isiyo ya kiserikalli inayofadhiriwa na chuo kikuu kimoja cha Marekani, ambao wao walifanyia maadhimishio yao pale katika viwanja vya mnazi mmoja. Ni kweli kwamba walikutana, wakasomeana risala kukumbushana kuhusu tatizo, mziki ukapigwa na burudani zingine mbalimbali kama vile mchezo wa mpira wa miguu zikaambatana na maadhimisho hayo.

Lakini hebu tujiulize maswali; Hivi tunahitaji kutumia fedha hizo za wahisani kwa ajili ya kukutana mnazi mmoja kukumbusha kuhusu Malaria? Ni nani hapa nchini ambaye hajui, au amesahau kwamba malaria ipo na kila baada ya sekunde tano inaua mtanzania mmoja, tena mama mjamzito na motto wa chini ya miaka mitano ndio wahanga wakubwa wa ugonjwa huu? Ni nani ambaye amewahi kwenda hospitali kupimwa malaria na hajawahi kuambia hata siku moja kwamba anaumwa malaria? Ni nani ambaye hana ndugu yake hata mmoja ambaye amekufa kwa ajili ya malaria? Sasa kwanini kila mwaka tuwe tunakutana mnazi mmoja KUKUMBUSHANA kwamba malaria tunayo na inaua? Au huo mpira wa miguu tunaoucheza hapo mnazi mmoja, unauhusiano gani na kutokomeza malaria hii inayoua maelfu ya watanzania wenzetu kila siku?

I wish kama wangekuwa wanatutangazia bajeti za sherehe hizo, lakini pia nadhani ni bora tu hawatutangazii pesa zilizotumika kufanyia sherehe hizo, maana kwetu sisi wenye ugonjwa wa moyo inawezekana kabisa tungepata mshtuko halafu tukatangulia mbele ya haki kabla ya siku zetu.

Lakini vipi kama tungeweza kuzitumia pesa hizo kuongeza madawa za malaria hospitalini na kwamba kila mwananchi aweze kupata dawa hizo bure? Au kwanini tusingezichangachanga pesa hizo ambazo serikali na taasisi zote nchi huzitumia ‘kukumbushiana’ na tukanunua na kunyunyizia dawa kwenye mazingira yetu kutokomeza kabisa hawa mbu wanaoeneza malaria??

Kinachokera zaidi ni kwamba tunakutana mnazi mmoja kukumbushana, halafu tunasahau kwamba ni mwanakijiji wa LUCHELELE huku ndie anaepoteza maisha kila kunapoitwa leo kwasababu ya malaria kwa kukosa dawa au kukosa sh. 500 kununulia chandalua cha haki punguzo na kushindwa kufika hospitalini kutokana na umbali wa hospitali ilipo.

Kama kweli tunataka kukumbushana, kwanini tusiwafate wanakijiji hawa waliowahanga wakubwa wa vitu hivi tunavyokumbushana, ili tukawakumbushe vizuri? Kwanini tufanyie Mnazi mmoja na kila mwaka, katikati ya watu wanaojua A-Z juu ya malaria, na wamezungukwa na zahanati na hospitali kibao wanazoweza kwenda na kupatiwa matibabu ya malaria na wenye uwezo wa kununua hizo dawa za malaria na vyandarua pia?

Wakati leo hii tumebaki kuhadithiana na kuwatamani nchi zingine za magharibi kwa kukomesha malaria, nasikitika kwamba tunasahau kwamba wao hawakuiondoa malaria kwa kukutana tu na kukumbushana! Ilifika mahali wakachoka kukumbushana, wakaamua kuingia vitani kwa dhati kupambana na malaria. Wakaamua ‘kujipigapiga’ vijesenti walivyokuwanavyo, wakanyunyizia dawa kuzunguka mazingira yao, wakateketeza mazalia yote ya mbu wanaoeneza malaria, na leo hii Malaria ni historia kwao!

Sasa hebu niwaulize watanzania wenzangu, kujikumbusha kwetu huku kusikoisha, ni kwamba bado hatujaichoka hii malaria? Hivi kweli tumeamua kuitokomeza? Au ndio niamini kwamba wapo wale wenzetu wanaomba malaria hii iendelee kuwatafuna watu, isiishe, kwa sababu wao malaria hii inawapatia wao kula kwa kufanya kazi kwenye NGO’s za kukutanisha watu manazi mmoja kukumbushana juu ya malaria?

Kinachonishangaza zaidi ni kwamba ndugu zetu kabisa wa Zanzibar malaria wameanza kuiona kama historia. Ukifungua mitandao mingi ihusuyo malaria, utaikuta Zanzibar miongoni mwa nchi chache sana duniani zinazopigiwa mfano kwa kuitokomeza malaria. Sasa kitu gani kinachotushinda sisi kuiga mfano wao?

Kiukweli sikupanga kabisa kuzungumzia maadhimisho ya Malaria, lakini wakati nilipokuwa naendelea kuandika, nikakumbushwa vitu hivi ambavyo huwa vinanikera kila ninapovisikia maskioni mwangu.

Kikubwa kabisa kilichonisukuma kuandika, ni kesho tunapotarajia kusherehekea siku ya mtoto wa Africa. Nikakumbuka mambo yale yale ya kukutana mnazi mmoja na kukumbushana kwamba watoto wetu wanaishi katika mazingira magumu, wanazurura mitaani wakiombaomba msaada, hawaendi shule, lakini kwani ni nani asiyeyajua haya? Na kwasababu sasa tumeshakumbushana vya kutosha, ni lini tutaingia kwa dhati kuyashughulikia matatizo yao kama jamii kwa ujumla, badala ya kuwa kila mwaka tunakutana mnazi mmoja kukumbushana?

Mwanza bila shaka ni moja kati ya miji mikubwa nchini mwetu yenye idadi kubwa sana ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Ukitembea karibu kila mtaa mjini, utakutana na angalau watoto wawili ambao wanaishi katika mazingira magumu.
Siku moja niliwahi kuwauliza watu wanaofanya biashara maeneo ya mjini, ambao pia waliwahi kuwauliza watoto wenyewe sababu za wao kuondoka nyumbani kwao na kuja mtaani. Japo si mara zote watoto hawa ni wa kweli, lakini mara nyingi sababu ambazo wamekuwa wakizitoa ni sababu ambazo ziko ndani kabisa ya uwezo wa jamii yetu kuzipatia ufumbuzi.

Wengi wao wamekuwa wakilalamikia wazazi wao wa kambo (wazazi wakufikia), hasa mama, ambao wamekuwa wakiwatesa bila ya baba yao kujali. Lakini pia wengine wamekuwa wakisema wazazi wao wote wawili kufariki kwa ugonjwa wa UKIMWI, na hivyo wameachwa bila mtu wa kuwatunza na sababu nyingine kama hizo.

Lakini watu wazima wengi amabo kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakifuatilia tatizo hili, wamekuwa wakitaja sababu kama kuwepo kwa shughuli za uvuvi (hasa hapa Mwanza) ambazo zinawashawishi watoto kukimbia kwao, wakitaka kuja kufanya shughuli hizo kujipatia pesa na matokeo yake wanashindwa kuzifanya, lakini pia watoto wengi wanakimbia nyumbani kwao kwasababu hawapendi kwenda shule na sababu nyingine nyingi.

Binafsi nikiziangalia sababu hizi, naona zipi ndani kabisa ya uwezo wa jamii. Ndio maana naendelea kujiuliza swali, KWANINI JAMII TUSIAMUE KUKOMESHA SABABU HIZI WATOTO WETU WARUDI KUISHI NYUMBANI, WALELEWE KATIKA MAZINGIRA MAZURI? Nani bado anataka kuendelea kukumbushwa juu ya mazingira magumu wanayoishi watoto?

Wakati umefika sasa jamii tuliangalie upya swala hili la maadhimisho, na kukumbushana, na tuone haja sasa ya kuendelea kukumbashana huku tukichukua hatua za kuyatatua matatizo yetu, badala ya kuendelea kukumbushana huku tatizo likiwa pale pale au linazidi kuongezeka.

Tanzania yetu itajengwa na sisi wenyewe watanzania. Hakuna muhisani atakayekuja kutujengea kama sisi wenyewe hatuoni bado uhitaji wa kuijenga!
TANZANIA BILA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU, INAWEZEKANA!

Friday, June 4, 2010

SACRIFICE IS WHAT WE NEED!

For many decades now, Tanzanians have been so badly longing for development. Every day we have been pointing out China as a good example of a fellow who happened to overtake us in progress right in front of our eyes.

It is said that when we got independence, China and Tanzania were on the same page as regards to economic development. But ironically, today how the world applauds China is completely different as to how it talks of our beautiful country, rich of natural resources.

While the former is now (almost) number one economic threat to a giant nation like United States of America, Tanzania is heading towards a peripheral; perhaps a symbol of those below the datum line and one of the biggest beggars to the United States and other powers of the like.

We seem not to be pleased with that and we try to ask some questions like, what is wrong with us? What can we do to get out of this snare?

But I really doubt whether we ask ourselves the right questions. If we are honest about the questions we are asking, or if we are really tired of being in this situation and that we really want to get out of it! Why do we still remain stunted? Our development is malnourished; it’s like a human being with a big head that does not correspond to the rest of the anatomy.

If you have ever hunted (as if I have) especially by using snares, you will agree with me that a trapped bird or animal does not just sit around relaxing, waiting to be taken. They always do something!

Now let’s talk about us, Tanzanians, can we really say that we are doing something to get us out of this ‘poverty snare’?

Besides, it seems it is a virtue in this country where husbands and fathers, who to a large extent are the main supporters of families, go drunk in the early morning hours and their kids get kicked of school for not paying tuition fee or school contribution. Yet we still dream of getting rid of the nick name ‘poor/third world country’ where her people live by less than a dollar per day.

It is in this country that employers take up people not because they qualify for the position but just because they are their nephews and nieces, as a result our production continues to derail day after day because of incompetency, while the corporate and government employers continue to lie to themselves about opening doors for economic competition with the East African federation and the globe at large.

This is the country that officials receive bribes to cover up an injustice case that eventually hurts the nation and absolutely nobody seems to care about it at all!

On the other hand, I am reminded of the story I read in a newspaper about one Asian leader who tossed himself from a mountain after learning that his fellow government officials found fraudulent evidence on a project he was assigned to administer. The step taken by the ex-president of South Korea is a deed which I find to display a high extent of personal consciousness over a public interest.

There are so many living examples that contradict our insincere desire to move forward towards the development we ‘sing’ of everyday.

The April 19 - 25th, 2010 East African Newspaper on its front story reported; “Tanzania has lost $ 8.9 billion over the past four decades through the illicit means – meaning that it leads the list of East African states that have lost billions of dollars to money laundering, tax evasion, government graft and other illegal operations, according to a report by a US-based financial watchdog group.” (Emphasis by the writer)

In another May 31- June 6, 2010 of The East African issue, the Newspaper again reported on its front page story; “Tanzania’s Ministry of Finance is in talks with local commercial banks to borrow up to $ 250 million to cover a deficit left by a recent withdrawal of support by donors” ( Emphasis by the writer)

Although the withdrawal of support by donors has not yet been officially confirmed as the result of carelessly spending of the government, but to a large extent it is believed so. The withdrawal from donors and the government’s scandal to lead in the list of East African states for money ‘terrorism’ is such a disgrace and stretches even further the hope for progress. On top of that it raises more questions as to when and what would be the remedy to the challenges of all three; political, social and economic spheres of the country.

I have to admit that I cannot be confident enough to mention that through my meditation of our bitter situation I found this or that to be a perfect start for addressing our problems. But as the saying goes ‘charity begins at home’! I myself as a journalist-to-be by profession, realizing the crucial role that this profession had, has and will continue to play in changing the society, have thought through and come up with some check notes for us practitioners as we determine to bring out what is good out of society.

Centuries ago, British historian, Lord Thomas Babington Macaulay, realizing the role of the media in changing the society, baptized the media as the Fourth Estate. In a society like ours, as Jenerali Ulimwengu once described it, “The Chief is always right, it’s his advisors who mislead him,” a slip of the government in its function is very possible and not-very-easy of the majority led to check in with it is a reality, the media is the only tool that can play a watchdog function.

History tells us that the very early tool of the independence fighters of many African countries used newspapers such as VOICE OF TANU (1954, WEST AFRICAN PILOT, ACCRA EVENING NEWS and MUIGMITHANIA the means said to had been very persuasive and uniting Africans for the fight of their independence. The role which its fruit is so evident that today every African country is politically free.

The power of the media can no way be sufficiently discussed in this brief summary, but examples such as that of revealing of RADAR, EPA and RICHMOND scandals, just to mention a few, are living testimonies of how if proficiently the media is used, can result into astounding domino effect, yes, even changing our pitiful situation. But how is the media situation itself?

A status of a media practitioner in Tanzania on the other side is not that of noble at all. The nicknames given to them such as machinga and kanjanja tells it all the exact perception that the people (whom could have trusted this vehicle for their redemption) have towards journalists.

They view them as the people who have lost their dignity and findings such as the submission of about 210 cases between 1997 and 2007 to the Arbitration Committee of the Media Council of Tanzania, the jailing of one of the prominent reporter in 1990’s accused of corruption and that of Jelly Murro alleged of corruption which is still on proceedings the proof of the status of the journalism legacy in the country.

Though the socialism ideology has in many cases been praised as the basis our unity, udugu and ujamaa it has also been a ‘veil of blunders’ in our society. I have always been wondering if one can testify a lie of his/her fellow students to have been done an assignment which he/she didn’t do just in the name of ‘friendship’, when will this person develop a gut of revealing evils by a society’s leader in the presence of a bribe worthy three years most Tanzania young journalists are paid?

Dr. Bernadine Mfumbusa asserts that ‘A habit is a settled or regula tendency or practice, which overtime becomes automatic. It is something that is acquired…. Journalists are expected to cultivate habits such as verifying facts before publication, ascertaining names of sources, editing news stories, and never telling a lie’

On the other hand a veteran DailyNews newspaper journalist Gabby Mgaya in his article ‘Journaists should be journalist’ at the column ‘FOURTH ESTATE’, Monday, May 31, 2010 adds that ‘….a good journalist (among many other factors he mentioned) is expected to be knowledgeable. This entails a lot of reading and listening – and analyzing issues…..’ A factor which in a 10 (most) journalist rarely 5 posses it. An incident that creates doubts if these journalists can really efficiently perform their duties.

While this fourth estate puts itself on self-check it is also important to turn to the spearheads of development, mostly government leaders. This side, as discussed earlier have some serious illness that they too need to work on, especially when they are brought fourth issues by the public through media that they need to work on.

I agree pretty much with Wangari Maathai, the 2004 Nobel Peace Laureate in his article ‘International Criminal Court belongs to us Africa’ in a May 24-30, 2010 The East African newspaper that; “….. if Africans are not ashamed of crimes (and even corruption) against their own people, neither the ICC nor any other governments can help them.”
As I mentioned area, while the culture of ‘Ujamaa’ and that of ‘Wazee’ has built us in so many ways, it has also destroyed us in so many ways. Most of our government leaders have not been ready to expose or deal sufficiently with their fellow or previous leaders when it comes to a need for legal measures to be taken for whatever evils they have done while in their positions.

In some countries, there are even laws that do not allow the outgoing leader to be taken to court for whatever blunder they have done when they were in the offices. Media in this case have done quite notable good job in revealing their evils, but the government seem to have not been taking the matters serious.

It is true that this kind of huge changes can not very easily made. Because a true salvation requires a sacrifice. As for the Christians’ belief of Christ’s sacrificial death for the salvation of the sinners, so is how I believe that for a true ‘salvation’ of our social-political and economic situation which will give birth to the true development we long and dream for, a sacrifice has to be made.

A sacrifice of even our dear ones who in one way or another have greatly contributed to our success, instead if we truly long for the salvation of our today and next generation, we shouldn’t be cowards but rather darers to face this development snare that have for decades shackled us.

Sunday, May 9, 2010

???

Months ago, somebody asked this question, but as Tanzanians, I think we still need to ask ourselves this same...;

WHAT IS OUR PROBLEM...?

Is it Our leaders? Effects of colonialism? Education system? or is it us, ourselves, tanzanians, ?

How and why exactly have we got where we are now...? Who is to blame for our situation?

Lets talk.....

Friday, May 7, 2010

Finally....

....I've opened a blog!

It has been quite sometime I've been thinking about starting a blog. And the biggest reason is the desire to inform! Thats ALL...
So many times I walk around I see many things and I'm like "people need to know about this!' and I ask myself, 'but how?' and the idea of a blog click in my head; 'through a blog!'
And now here I am today, with my blog...

I've been having hrd time deciding which language should I use, English or Swahili? I love English and I would really love my English speaking folks get informed also of what I'm reporting, but again, I'm a native swahili speaker so I'm more confortable in swahili than English (and beside, I dont have that very good English and I dont wanna mess up people's language) But anyway, will try my level best to use all languages. So dont be supprised when you'll find two language! And sorry if you'll not be able to understand one of them.
Otherwise, i would really appreciate receiving comments and posts as well.

Welcome all and let us build NYUMBANI KWETU TZ!